
Baada
 ya kikao cha karibia masaa 4 au zaidi viongozi wa vilabu 14 
vinavyoshiriki ligi kuu ya Tanzania bara walifikia maamuzi ya kuanzishwa
 kwa kampuni itayoendesha ligi kuanzia msimu ujao.
Kikao
 hicho kilichofanyika katika hoteli ya JB Del-monte (zamani Paradise) @ 
Benjamin Mkapa Tower kilihudhuriwa na viongozi 13 kati ya 14 wa vilabu 
vya ligi kuu isipokuwa Kagera Sugar waliotoa udhuru lakini wakisema 
wataunga mkono maamuzi yatakayotolewa

Katika
 kikao hicho maamuzi yaliyotolewa ni kwamba uanzishwe mchakato wa 
kuwezesha usajili wa kampuni ambayo itaendesha ligi hiyo, huku Makamu 
mwenyekiti wa Simba Godfrey Nyange Kaburu akiteuliwa kuwa mwenyekiti wa 
kamati hiyo, Celestine Mwesiga katibu mkuu Yanga-Makamu mwenyekiti, Meja
 Ruta wa Ruvu Shooting- akiteuliwa Katibu wa hiyo kamati, na Shani wa 
Azam FC na Evadius Mtawala wa Simba wakiwa wajumbe, ambao wote kwa 
pamoja watashugulikia mchakato wa kupatikana kwa usajili wa kampuni 
hiyo.

“Dauda alialikwa na viongozi wa vilabu kutoa mawazo yangu juu mchakato mzima wa kuundwa kwa kampuni itayoendesha ligi kuu.”
Pia
 viongozi hao wa vilabu 13 vya ligi kuu walitoa shukrani sana kwa vyombo
 vya habari hususani kwa watangazaji wa vipindi vya Sports extra na 
Sports Bar kutoka Clouds media group kwa kuwa watu wa kwanza kuanzisha 
na kusimamia mjadala wa kuanzishwa kwa kampuni ya kuendesha ligi kuu 
Tanzania bara.
chanzo na shaffih dauda wa
        www.shaffihdauda.com
No comments:
Post a Comment