Dec 30, 2011

BONDE FC KUANZA MAZOEZI SIKU YA JUMATATU

  na shabani kpl

Juu na chini ni vijana wa bonde fc wakijifua kabla ya mechi















Timu ya Bonde fc inawatangazia mashabiki na wanachama wake kuwa itaanza  mazoezi rasmi siku ya jumatatu. Akiongea na chumba cha habari kocha mkuu wa Bonde fc ndugu Issa Joseph  amesema kuwa wataanza mazoezi rasmi siku hiyo ikiwa ni baada ya mapumziko ya sikukuu xmss na mwaka mpya hata hivyo kocha huyo alizidi kukipasha chumba cha habari kuwa mazoezi hayo watakuwa wakifanyia katika uwanja Magomeni Tuliani kufuatia uwanja wao wa nyumani kukumbwa na mafuriko hivyo amewahasa wachezaji kufika mazoezini siku hiyo pia wanawakaribisha mashabiki wa soka kuja kushuhudia 
 

Dec 14, 2011

Kampuni ya 2F CO.LTD YAJITOSA KUIDHAMINI BONDE KIDS

 Picha juu na china mmoja wa wakurugenzi wa 2F CO.LTD mwenye kanzu akiwa  na viongozi pamoja na wachezaji wa Bonde Fc siku ambapo Bonde fc ilishinda mechi yake ya nusu fainali .
2F CO.LTD imejitolea kuisaidia timu ya Bonde Kids.  Itakuwa ikiisaidia Bonde Kids katika vifaa vya michezo zikiwemo jezi na masuala mbalimbali yanayohusu kuindeleza timu 
Pia kampuni ya 2F CO.LTD kupitia kwa mmoja wa wakurugenzi wake Bwana SALM NGINGO pia imewataka watu wengine wenye uwezo kujitokeza katika kuisaidia timu kwani kusaidia timu kama hizi ndio kusaidia kukuza soka la nchi yetu. Nao uongozi mzima wa Bonde Kids unatoa shukrani kwa kampuni ya 2F CO.LTD kwa uamuzi wao wa kuamua kidhamini timu yao pia wanawaomba watu wenye nia nzuri na soka la vijana kujitokeza kuzisaidia timu kama hizi zenye malengo ya kuinua soka la vijana.

SIKU BONDE FC ILIPOINGIA NUSU FAINALI TA TEWA CUP

 Kikosi cha Bonde Fc kikiwa katika ukaguzi kabla ya mechi ya nusu fainali  dhidi ya Makumbusho Talent Bonde fc iliibuka na ushindi wa 6-5 magoli yaliyopatikana kwa njia ya kupigiana mikwaju ya penati baada ya kutoka nguvu sawa katika muda wa kwaida chini ni kikosi kamili cha Bonde Fc na makocha wao .kulia ni kocha mkuu Issa Joseph na kushoto ni Rashid Banda kocha msaidizi.  

Hiki ni kikosi cha Makumbusho Tarent ambacho kilifungwa na Bonde fc katika mechi ya nusu fainali

Dec 13, 2011

BONDE FC YAJITOA MASHINDANO YA DAYOSA

 
 Siku Mwinyimaji Tambaza alipoitembelea Bonde fc mazoezini hakuna alietegemea kama iko siku atatugeuka
 
 
 
 
Timu ya Bonde Fc inawatangazia mashabiki wake kuwa imeamua kujitoa katika michuano ya DAYOSA kutokana na ukiritimba na ufisadi unaofanywa na katibu wa chama hicho ndugu Mwinyimaji Tambaza kwa kitendo chake cha kuzifungia timu za Shein Rangers na Bonde fc zisishiriki michuano ya aina yoyote inayoandaliwa na chama hicho na hata kutotakiwa kucheza mechi za kirafiki na timu yeyote unayoshiriki michuano inayoandaliwa na chama hicho sasa tunajiuliza hivi huyu jamaa kazi yake kuendeleza soka au kuua vipaji vya vijana.kwani alikwisha wahi kumshawishi ndugu Ibrahimu Tewa kuifuta Shein katika michuano ya TEWA CUP baada ya shein kugoma kushiriki michuano ya DAYOSA inayoendelea kutokana na ukilitimba wa kiongozi huyu