Sep 29, 2011

ABOODMSUNI NA SOKA LA BONGO: YANGA NA MWENDELEZO WA PROJECT ZAO

ABOODMSUNI NA SOKA LA BONGO: YANGA NA MWENDELEZO WA PROJECT ZAO: Baada ya Azam FC kuanza kuutumia uwanja wake wa Azam uliopo maeneo ya Chamanzi umeamsha project iliyokuwa imesimama pale Jangwani. Katika ...

ABOODMSUNI NA SOKA LA BONGO: ASAMOAH AFUNGUKA, YANGA WAWASAMBARATISHA WAGOSI

ABOODMSUNI NA SOKA LA BONGO: ASAMOAH AFUNGUKA, YANGA WAWASAMBARATISHA WAGOSI: Mshambuliaji wakimataifa toka Ghana anaekipiga kwa mabingwa wa Tanzania Bara Yanga, Kenneth Asamoah leo kafunguka kwenye michuano ya ligi ku...

ABOODMSUNI NA SOKA LA BONGO: CECAFA wazialika Nigeria, Cameroon nchini Tanzania...

ABOODMSUNI NA SOKA LA BONGO: CECAFA wazialika Nigeria, Cameroon nchini Tanzania...: TIMU za soka za Cameroon na Nigeria zinatarajiwa kushiriki michuano ya Kombe la Chalenji inayoandaliwa na Baraza la Vyama vya soka Afrika Ma...

ABOODMSUNI NA SOKA LA BONGO: Sunzu fiti, Machaku aondolewa POP

ABOODMSUNI NA SOKA LA BONGO: Sunzu fiti, Machaku aondolewa POP: SIMBA imepata matumaini ya kuendelea kufanya vema katika Ligi Kuu soka Tanzania Bara, baada ya nyota wake waliokuwa majeruhi akiwemo kiungo ...

Sep 28, 2011

KIKOSI CHA TAIFA STARS KWA AJILI YA MECHI YA MOROCCO



Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen leo (Septemba 27 mwaka huu) ametangaza kikosi cha wachezaji 23 kwa ajili ya mechi ya mwisho ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani dhidi ya Morocco.
Kikosi hicho kitaingia kambini Septemba 29 mwaka huu jijini Dar es Salaam, na kinatarajiwa kuondoka nchini Oktoba 6 mwaka huu kwenda Casablanca, Morocco kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Oktoba 9 mwaka huu kwenye mji wa Marrakech.
Wachezaji walioitwa ni makipa Shabani Dihile (JKT Ruvu Stars), Juma Kaseja (Simba) na Shabani Kado (Yanga).
Mabeki wa pembeni ni nahodha Shadrack Nsajigwa (Yanga), Erasto Nyoni (Azam), Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya) na Amir Maftah (Simba).
Mabeki wa kati ni Aggrey Morris (Azam), Juma Nyoso (Simba) na Victor Costa (Simba).
Viungo wakabaji ni Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway), Nurdin Bakari (Yanga), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar) na Jabir Aziz (Azam).
Viungo washambuliaji ni Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada), Mrisho Ngassa (Azam) na Ramadhan Chombo (Azam).
Washambuliaji ni Abdi Kassim (DT Long An, Vietnam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Dan Mrwanda (DT Long An, Vietnam), Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden), John Bocco (Azam) na Hussein Javu (Mtibwa Sugar).
 chanzo na Shaffih Dauda wa 
www.shaffih.blogspot.com

Sep 26, 2011

Bonde fc yaichapa Magomeni kids

Vijana wa Bonde fc wakipasha kabla ya mechi kuanza. vijana hawa wa Bonde fc waliibuka na ushindi mnono wa gili 2-0 dhidi ya Magomeni kids mechi ilichezwa katika uwanja wa magomeni barafu hapo jana tarehe 25/09/2011

Sep 24, 2011

Timu ya Bonde fc inaendelea na mazoezi kama kawida



VIJANA WAKIMSIKILIZA MWALIMU WAO CHIDI BANDA  HAPA

MAKIPA NAO WAKIENDELEA NA MAZOEZI YAO




VIJANA WAKIPASHA

Sep 20, 2011

Kama ulidhani unaujua utani, basi sikia hii

Mwamuzi Howad Webb, anapochaguliwa kuwa mchezaji bora kuwahi kuichezea United.
Katika hali ya kustaajabisha sana, baadhi ya mashabiki wa soka kutoka kona mbalimbali za dunia wamemchagua mwamuzi Howad Webb kuwa ndio mchezaji bora kabisa wa sasa wa kikosi cha Manchester United chini ya kocha Alex Ferguson, ikiwa ni dakika chache sana toka kocha huyo mkongwe kumfananisha mshambuliaji wake Wayne Rooney sawa na gwiji wa soka Pele.
Mashabiki hao wamefanya hivyo kupitia kura ya maoni iliyokuwa ikiendeshwa na mtandao maarufu wa habari za michezo duniani wa TalkSports, ambao katika ukurasa wao wa Facebook, waliendesha kura hiyo kwa kuuliza “Fergie amemfananisha Wayne Rooney na Pele, lakini unadhani ni nani mchezaji bora kabisa wa Manchester United?”
Kwenye kura hiyo, mtandao huo uliainisha majina ya wachezaji kadhaa wakiwemo Bobby Chalton, Ryan Giggs, Eric Cantona, Eric Djemba Djemba, Duncan Edwards, Wayne Rooney, Cristiano Ronaldo, Paul Scholes na wengineo wengi ambapo katika hali ya kustaajabisha wapiga kura walimtaja Howad Webb kama mchezaji bora kwa zaidi ya asilimia 48, akiwaacha mbali kweli magwiji wa ukweli.
Webb alipata asilimia 48, akifuatiwa katika nafasi ya pili na Bobby Chalton (20%), Ryan Giggs akishika nafasi ya tatu.

Kazi kweli kweli…

Giggs aweka rekodi United wakianza kwa sare

Ryan Giggs, alikuwa na usiku wa aina yake baada ya kufanikiwa kujiwekea historia ya kuwa mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi kuwahi kufunga katika michuano ya klabu bingwa Ulaya na kuisaidia klabu yake ya Manchester United kufanikiwa kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya Benfica ya Ureno.
Katika pambano hilo ambalo lilikuwa wazi kwa timu zote huku yeyote kati ya timu hizo mbili akionekana angeweza kuibuka na ushindi ndani ya dakika tisini za mchezo, wenyeji walitangulia kufunga kupitia kwa Oscar Cardozo kunako dakika ya 24 ya mchezo.
Alifunga bao hilo baada ya kutumia makosa ya mabeki wa United, ambapo aliachia shuti kali la umbali wa takriban mita 18 hivi lililomshinda mlinda mlango wa United na baada ya hapo wenyeji wakaonekana kama wangeongeza bao wakati wowote.
Hata hivyo, dakika chache kabla ya mapumziko, Ryan Giggs alipokea pasi safi toka wingi ya kulia mwa uwanja kabla ya kukokota mpira huku akiwadhibiti mabeki kadhaa wa Benfica na kisha kuachia mkwaju safi na kuandika bao la kusawazisha, na matokeo hayo yakasimama hivyo hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili kilishuhudia timu zote zikifanya mabadiliko kadhaa sanjari na kucheza kandanda safi lakini zaidi ya kosakosa kadhaa kwa kila upande, hakuna timu iliyoweza kuliona lango la mwenzie na hivyo hadi mwisho wa mchezo Benfica 1-1 United.
Ryan Giggs awa mchezaji mkongwe zaidi kufunga katika ligi ya mabingwa Ulaya
Bao la Giggs linamfanya aweke rekodi ya kuwa mchezaji mkongwe zaidi kufunga katika michuano hiyo akiwa na umri wa miaka 37 na siku 289, ambapo pia anampita mkongwe Raul Gonzalez kwa kuwa mchezaji aliyefunga katika misimu mingi zaidi ya michuano hiyo, akiwa amefikisha misimu 16 hivi sasa.
Wakati United wakiambulia sare ya ugenini, jirani zao Manchester City nao walijikuta wakiambulia sare ya nyumbani dhidi ya Napoli kwenye mechi ambayo wageni Napoli walitangulia kufunga kupitia kwa Edinson Cavani lakini wenyeji wakajitutumua na kusawazisha kupitia kwa Aleksander Kolarov dakika chache baadae.
Kule nchini Uholanzi, Ajax walibanwa vilivyo na waliokuwa wageni wao Lyon ya kutokea nchini Ufaransa na kuambulia sare ya bila kufungana lakini miamba ya Hispania Real Madrid wakianza michuano hiyo vyema baada ya kuchomoza na ushindi wa bao 1-0 wa ugenini kwenye uwanja wa Dinamo Zagreb, bao pekee la mchezo huo likiwekwa kimiani na Angel Di Maria.
Mechi zingine za usiku huu zimeshuhudia FC Basle wakiibuka na ushindi wa bao 2-1 dhidi ya SC Otelul Galati, huku Inter Milan wakianza vibaya baada ya kukubali kichapo cha nyumbani cha bao 1-0 toka kwa Trabzonspor.
Nao wafaransa Lille wakiwa nyumbani wakaambulia sare ya bao 2-2 dhidi ya CSKA Moscow Ilhali Villarreal wakiwaruhusu wageni wao Bayern Munich kuwaadhiri nyumbani kwa kichapo cha bao 2-0

Maftah- Yanga walitaka kuua kipaji changu


Maftah- Yanga walitaka kuua kipaji changu


Amir Maftah, akiwa katika jezi ya Simba
BEKI wa kushoto wa timu ya taifa, Taifa Stars na Klabu ya Simba, Amir Maftah ameamua kuweka wazi kile kilichomtokea wakati akiwachezea watoto wa Jangwani, Yanga Afrika.
Katika mahojiano maalumu na safu hii, Maftah anasema kwamba ana mshukuru Mungu kwa sasa yupo kwenye timu ambayo ina viongozi wanaotambua mchango wake na wasio na mizengwe kama ilivyokuwa kwa upande wa Yanga.
Anasema; “Kwa hakika kabisa naamini hivi sasa nisingekuwepo tena kwenye ulimwengu wa soka, kwani pale Yanga nilifanyiwa mambo ya ajabu mno yaliyokuwa yanatishia majaliwa yangu ya baadaye.”
Anasema licha ya kuichezea Yanga kwa moyo wake wote na mapenzi makubwa aliyokuwa nayo, lakini alishangaa kujikuta akihusishwa na kuihujumu timu hiyo.
“Kiukweli, mimi nilikuwa naipenda Yanga tangu nikiwa mdogo kabisa, malengo yangu yalikuwa ni kuhakikisha siku moja nakuja kuichezea.
“Mapenzi na Yanga yalikuwa ni ya kutoka moyoni kabisa, lakini niliyoyakuta, na mizengwe niliyofanyiwa, kwa hakika kabisa naweza kusema hakuna klabu ninayoichukia kama Yanga.
“Hata ninapocheza dhidi ya Yanga huwa nafurahi mno kuhakikisha tumewanyanyasa tunavyotaka na kuwafunga, kwani siipendi kabisa Yanga.
“Na katika kila mchezo nitahakikisha nacheza kufa au kupona kuhakikisha tu furaha nyangu ya kulipiza kisasi cha waliyonifanyia inatimia.”
Anasema wakati akiwa katika Klabu ya Mtibwa ya Manungu Turiani mkoani Morogoro, Simba walimfuata mara kadhaa kwa ajili ya kutaka kumsajili, lakini yeye akaikataa ofa hiyo.
“Niliikataa Simba kwa sababu tu nilikuwa na mapenzi makubwa na Yanga, hivyo sikutaka kuwachezea watoto hao wa Msimbazi, kwani akili yangu ilikuwa kwa watoto wa Jangwani.
“Na hata Yanga waliponifuata kwa ajili ya kutaka kunisajili sikuwa na kipingamizi, kwa sababu tayari walikuwa moyoni mwangu, hivyo nikatua kwao.” Maftah anasema licha ya kucheza kwa kujituma wakati akiwa na Yanga, lakini alishangaa kuona mizengwe ya hapa na pale kutoka kwa viongozi wa timu hiyo.
Anasema awali alichukulia ni mambo ya kawaida, lakini siku jinsi zilivyokuwa zinakwenda, akajiridhisha kwamba viongozi hao hawakuwa na nia nzuri na yeye.
“Ilifikia kipindi eti nikawa nashutumiwa kwamba mimi naihujumu Yanga kwa sababu ni mpenzi wa Simba, kitu ambacho kwangu kilikuwa kigeni kabisa kukisikia, lakini niliamua kuvumilia.
“Hata hivyo, kuna siku nitamuweka hadharani kiongozi mmoja wa Yanga ambaye alisababisha matatizo yote haya kiasi kwamba hadi mimi kuonekana msaliti.” Maftah anasema baada ya kuachwa na Yanga katika mazingira ya kutatanisha, alikuwa na wakati mgumu mno kwenye mustakabali wa maisha yake ya soka.
“Mimi ajira yangu ni soka. Soka ndiyo ninayoitegemea kuendesha maisha yangu ya kila siku pamoja na familia yangu, hivyo kuacha soka maana yake ni kwamba nakosa ajira. “Nilisota, huku nikijaribu kuangalia muelekeo utakuwaje, lakini namshukuru Mungu kwamba Simba wakaniona na wakanisajili kwa mkataba mnono.”
Anasema baada ya kutua Simba aliona mambo mengi ni tofauti, kwani viongozi wake walikuwa wanaonyesha kumjali kila mchezaji na hakuna mizengwe yoyote inamkera.
“Kwa uhakika kabisa naweza kusema hapa Simba nimefika, kwani viongozi wake wanawajali wachezaji na hata kiwango changu kimezidi kuimarika kwa sababu akili yangu yote ipo kwa ajili ya kuhakikisha inafanya vizuri katika kila mchezo.
“Simba wananilipa dola 600 kwa mwezi (sawa na zaidi ya shilingi 900,000) ambazo kwangu zinanitosha kabisa, hasa ukizingatia kwamba tunapata posho katika kila mechi, hivyo sina tatizo.”
Katika kuonesha shukrani zake, Maftah anasema kwamba amekuwa anajifua mno kivyake kuhakikisha kwamba anaendelea kuwa fiti ili kuweza kucheza katika kiwango cha juu kabisa.
Anasema hatarajii kuichezea timu nyingine kwa hapa Tanzania, kwani iwapo ataondoka Simba ndiyo utakuwa mwisho wake kama hatakuwa amepata timu nje ya nchi.
“Kwa kweli kwa upande wangu nikitoka hapa Simba, sina mpango wa kucheza katika timu yoyote ya hapa Tanzania, kwani kama sitapata timu ya nje ya nchi basi huo utakuwa ni mwisho wangu wa kucheza soka.”
Maisha kwenye Filamu Aidha Maftah anasema kwamba yupo kwenye hatua za mwisho za kukamilisha filamu yake inayozungumzia ukweli halisi wa soka la Tanzania (A True Story of Tanzanian Football).
Anasema kwenye filamu hiyo ataonesha matukio yote halisi ya mwenendo wa mchezo huo nchini pamoja na mwendendo wa klabu zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara.
“Humo kutakuwa na kila kitu kinachohusu maisha ya soka la Tanzania pamoja na historia yangu nilikozaliwa na nilikoanza kucheza soka.
“Pia nitazungumzia kwa kina yale yote yaliyonitokea katika maisha yangu ya soka kwa uhalisia wote.”
Anasema katika filamu hiyo atamshirikisha gwiji wa soka la zamani hapa nchini Zamoyoni Mogella pamoja na wasanii wengine ambao hakuwa tayari kuwataja kwa sababu bado hajakamilisha nao mazungumzo.
“Kutakuwa na watu wengi kwenye filamu hii ambayo inatengenezwa na kampuni ya Asaa chini ya Meneja wangu, Imam Maunda.”

Sep 17, 2011

Yanga yaona mwezi

Yanga yaona mwezi


Rashid Gumbo
Jesca Nangawe
MABINGWA watetezi, Yanga jana walipata ushindi wao wa kwanza kwenye Ligi Kuu baada ya kuichapa African Lyon kwa mabao 2-1 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Azam, Chamazi jijini Dar es Salaam.
Mashabiki wa Yanga waliokuwa na hamu ya kuona timu yao ikishinda mchezo huo walisubiri kwa dakika 35, mpaka mshambuliaji wa kimataifa wa zamani wa Zambia, Davies Mwape alipofunga bao la kuongoza, lakini Lyon walisawazisha bao hilo kupitia kwa Hamis Shengo kabla ya Rashid Gumbo wa Yanga aliyeingia akitokea benchi kufunga bao la ushindi katika dakika ya 63.
Kwa matokeo hayo Yanga imejinasua mkiani kwa kufikisha pointi sita katika michezo mitano na kurudisha faraja kwa mashabiki wao kabla ya mechi ya Jumapili dhidi ya Azam itakayofanyika kwenye Uwanja wa Taifa.
Pamoja na rekodi mbaya ya utovu wa nidhamu kwa timu za Ligi Kuu msimu huu jana mwamuzi Mathew Akrama wa Mwanza alichezesha mechi bila ya kuonyesha kadi kwa mchezaji yeyote.
Mchezo ulianza kwa kasi na katika dakika ya 4, Sino Agustino alifanikiwa kuunganisha vizuri krosi ya Seleman Kassim, lakini shuti lake liligonga mwamba na kurudi uwanjani.
Yanga ilijibu mapigo katika dakika ya 10 na 14 kupitia kwa Mwape aliyeshindwa kumalizia nafasi mbili baada ya kupigiwa pasi nzuri na  Nurdin Bakari na Shamte.
Bao la kwanza la Yanga lilipatikana baada ya  Pius Kisambale kupiga pasi ndefu kutoka katikati ya uwanja ambayo ilitua kwa Shamte Ally aliyemtengenezea nafasi Mwape ambaye  aliusukuma mpira wavuni katika dakika ya 35 na kuamsha shangwe kwa wanajangwani.
Dakika tano baadaye, Kassim wa Lyon aliwatoka mabeki wa Yanga na kipa Berko na kupiga shuti golini, lakini Juma Seif alifanya kazi ya ziada kuwahi mpira huo na kuutoa nje.Ikiwa inaonekana timu hizo zitaenda mapumziko huku Yanga ikiongoza kwa bao moja, Hamis Shengo aliisawazishia Lyon kwa mpira wa adhabu alioupiga na kwenda moja kwa moja wavuni na kumwacha Berko asijue la kufanya.
Kabla ya kufungwa bao hilo katika dakika ya 42, beki wa Yanga, Bakari Mbegu alimchezea vibaya kiungo Kassim nje kidogo ya eneo la 18, faulo ambayo ilitoa nafasi kwa vijana wa Lyon  kupata sare 1-1 hadi mapumziko.Kipindi cha pili Yanga ilianza kwa kasi na katika dakika ya 47, Pius Kisambale alikosa bao kwa shuti lake kupanguliwa na kipa Juma Abdul na kutoka nje.
Kocha Sam Timbe aliwapumzisha Shamte, Kigi Makasi na Juma Seif na kuwaingiza Kenneth Asamoah, Rashid Gumbo na Godfrey Bonny mabadiliko ambayo yaliisaidia Yanga.
Mabadiliko hayo yaliisaidia Yanga kwa sababu Gumbo aliyechukua nafasi ya Kigi aliipatia Yanga bao la pili katika dakika ya 63 kwa shuti la umbali wa mita 32, lililomshinda kipa wa Lyon, Abdul.Washambuliaji wa Lyon, Adam Kingwande na Agustino Sino watajilaumu wenyewe kwa kupoteza nafasi nyingi za kufunga katika mechi hiyo.
Katika mechi hiyo pia Gumbo alipiga shuti kali ambalo liligonga mwamba katika dakika ya 71 na kutoka vile vile Kenneth Asamoah alishindwa kumalizia pasi Kisambale akiwa ndani ya 18. Katika mechi hiyo kocha wa Lyon alifanya mabadiliko mapema, ambapo katika dakika ya 16 alimtoa Benedictor Jacob na kumwingiza Sammy Kessy pia baadaye alimtoa Kessy na kumwigiza Jacob Masawe.
Licha ya kuwapo ulinzi mkali kwenye uwanja wa Azam, wapo baadhi ya mashabiki waliruka ukuta ambao sio mrefu sana na kuingia uwanjani.Yanga: Yaw Berko, Shadrack Nsajigwa, Abuu Zuberi, Bakari Mbegu, Chacha Marwa, Juma Seif, Shamte Ally, Nurdin Bakari, Davis Mwape, Pius Kisambale na Kigi Makasi.
African Lyon: Juma Abdul, Aziz Sibo, Hamis Shengo, Shaban Aboma, Hamis Yusuph, Razaki Khalfan, Adam Kingwande, Seleman Kassim, Benedictor Jacob, Hood Mayanja na Agustino Sino.

MSIMAMO WA LIGI KUU BONGO

msimamo wa ligi kuu ndo huo:
nfs timu      chz shd sul ptz fga fgw tmg pts
1. simba sc    5    4   1   0    5     0     4    13
2. jkt ruvu     5    2   3   0    8    4      4      9
3. azam fc     5    2   2   1    4    2      2      8
4. moro utd   5    2   2   1    7    6      1      8
5. mtibwa      5    2   2   1    4    3      1      8
6. toto           5    2    1   2    7    5      2      7
7. madume    5    1    3   1    4    4      0      6
8. jkt oljoro   5    1    3   1     3    4     1       6
9. a. lyon       5    1    2   2     3   4      1      5                                          k. sugar          5    0    4   1    6    7      1      4                                         10. R.shooting 5  0   4   1      3    4     -1     4
12. c. union    5   1    1   3     3    7     -4      4
13. v. squad    5   1    1   3     3    8     -5      4
14. p. dodoma 5 0     3   2     3    5     -2      3

mechi za leo ni:
ruvu shooting v coastal union
toto african v jkt ruvu
villa squad v mtibwa sugar

Sep 15, 2011

Sep 13, 2011

vijana wakipasha misuri







VIJANA WAKIPASHA MISURI KABLA YA MECHI

siku under 14 ilipokwenda jipima nguvu na leaders kids





Hapa kabla ya kuhailishwa kwa mechi kati ya bonde kids dhidi ya leaders kids hapo jumamosi mechi hii iliahilishwa kwa sababu ya mama Salma kikwete kuwa na mkutano na akinamama ndani ya viwanja vya leaders

Sep 7, 2011

baada ya kuchukua ubingwa wa eid el fitri sasa timu inaendelea jifua


Timu ya bonde fc inaendelea na mazoezi yake kama kawaida katika uwanja wake wa nyumbani ili kujiwinda na michuanoi ya ligi ya tanzania betting inayoendelea katika viwanja vya garden kinondoni

Sep 3, 2011

Arsenal yawa klabu ya mfano Ulaya

Michel Platini, raisi wa UEFA ambaye anataka kuona vilabu vinaacha tabia ya kununua mafaanikio kwa kutumia fedha za wafanyibiashar
Wakati mamilioni ya mashabiki wa klabu mbalimbali za soka barani Ulaya wakiendelea kufurahia namna ambavyo timu zao zinamwaga mapesa kwa ajili ya kufanya usajili wa wachezaji wakali na hivyo kuongeza uimara wa vikosi vyao kila msimu wa usajili unavyowadia, Michael Platini, ametangaza  kuwa kiama cha vilabu vyote vinavyonunua mafanikio kwa kutumia jeuri ya fedha za wamiliki wao, kiko palepale na hakikwepeki.
Raisi huyo wa Shirikisho la Vyama vya soka barani Ulaya (UEFA), akiongea kwenye mkutano uliofanyika mjini Zurich jana, alisema kuwa, mpango wa kuvidhibiti vilabu ambavyo vimekuwa vikifanya matumizi makubwa ambayo ni nje ya uwezo wake wa uzalishaji, uko palepale na kwamba utaanza kutumika kwenye msimu wa mwaka 2012/13, kama ambavyo imeshakubaliwa.
Chini ya mpango huo, vilabu havitaruhusiwa kufanya manunuzi ya wachezaji au kulipa mishahara mikubwa kwa wachezaji wao zaidi ya kile klabu inachoingiza kama mapato yake kutokana na mikataba mbalimbali ya kibiashara na vyanzo vyao vya mapato na kwamba vilabu ambavyo vitashindwa kutimiza sharti hilo, vitafungiwa kushiriki michuano yoyote ya Ulaya katika ngazi ya vilabu.
Akizungumza katika mkutano huo, Platini, gwiji wa zamani katika kikosi cha Ufaransa na vilabu mbalimbali alitolea mfano wa klabu ya soka ya Arsenal, ambayo alisema kuwa miaka kumi iliyopita, mzunguko wake wa fedha kwa mwaka ulikuwa chini sana kiasi cha kupitwa na vilabu kama Chelsea, Liverpool na Newcastle, lakini kutokana na mipango mizuri na matumizi sahihi ya fedha, leo hii klabu hiyo imekuwa juu ya vilabu hivyo kwa karibu mara mbili kiuchumi.

Mkali wa Arsenal aanza na hat-trick

Chu-Young Park
Mshambuliaji mpya wa Arsenal Chu-Young Park, amesherehekea kutimia kwa ndoto yake ya kuwachezea washika bunduki hao wa London, kwa kuiongoza nchi yake ya Korea Kusini kuibuka na ushindi wa bao 6-0 dhidi ya Lebanon, katika michuano ya kuwania kufuzu fainali zijazo za kombe la dunia.
Park, ambaye alitua Arsenal hivi karibuni akitokea Monaco ya Ufaransa, aliwaonyesha mashabiki wa Arsenal kuwa huenda akawa tiba ya timu yao kushindwa kupata mabao katika baadhi ya nyakati, baada ya kutikisa nyavu mara tatu kwenye mechi hiyo iliyofanyika leo huko nchini kwao.
Pak, alifunga mabao yake kunako dakika za 8, 45 na 67, huku mabao mengine yakiwekwa nyavuni na Don Won Ji (66 na 85) pamoja na Jung Woo Kim, aliyefunga bao moja kunako dakika ya 82.

Yossi Benayoun amwaga wino Arsenal

Yossi Benayoun, anaelezwa kuwa mchezaji ambaye ataleta kitu muhimu kwa Arsenal kutokana na aina yake ya uchezaji na aina ya uchezaji wa Arsenal kama timu
Hatimaye Arsene Wenger ameibuka na kicheko dhidi ya mahasimu wake Liverpool na Tottenham Hotspurs, baada ya kufanikiwa kuinasa saini ya kiungo Yossi Benayoun, toka Chelsea.
Dilila kumsaini mchezaji huyo ambalo lilionekana kushika kasi saa chache zilizopita baada ya Arsenal kuelekea kumkosa Mikel Arteta, lilikuwa likiendeshwa kimya kimya sana ukiachilia mbali taarifa zilizokuwa zikitolewa na mchezaji huyo mwenyewe kupitia ukurasa wake wa Twitter.
Haijawekwa wazi dau lake na lakini inaelezwa kuwa amesaini kwa mkopo wa muda mrefu ambao unaweza kugeuzwa kuwa wa kudumu na bila shaka hizi ni habari njema sana kwa mashabiki wa Arsenal ambao walichokuwa wakiangalia ni kuimarishwa kwa kikosi chao kabla ya dirisha la usajili kufungwa.
Benayoun mwenyewe amezungumzia usajili huo kwa ufupi sana katika ukurasa wake wa Twitter ambako ameandika “I sign with arsenal,very happy and excited about it,but now my head is only in the game against grecce on friday,thanks for the support”.
Je, ni nani atasaini dakika hizi takriban 20 zilizobaki? Ni Arteta, ambaye amelazimisha Everton wamuachie baada ya awali kukataliwa kwa maombi ya Wenger au basi ndio kocha huyo Mfaransa kafunga duka? 

Sep 2, 2011

Timu ya Bonde fc inawatangazia kuwa kesho itacheza mechi ya nusu fainali katika uwanja wa Mwenge shouting

Kaptein wa Bonde fc Swalehe( Canavaro) amewahaidi mashabiki wa Bonde fc kuwa kesho lazima aingoze timu yake kutinga hatua ya  fainali katika mechi ya nusu fainali itakayochezwa hapo katika viwanja vya Mwenge shoutting watu wote mnakaribishwa

AFRICAN LYON WASHINDWA TAMBA MBELE YA COASTAL UNION

AFRICAN LYON WAPOTEA CHAMANZI

African lyon ya Mbagala wakiwa katika uwanja wa Azam uliopo Chamanzi jana walitoka mikono mitupu baada ya Coastal union kunyakuwa point zote 3 katika muendelezo wa Ligi kuu ya Vodacom.

African lyon wakiwa wenyeji wa Coastal union ya Tanga ja walishindwa kutamba na kuwaruhusu wagosi kuondoka na ushindi wa goli moja bila, goli likifungwa na Salum Azizi Gilla katika dakika ya 20 ya mchezo.

Kutokana na Ushindi huo Coastal union imevikisha point 4 na kupanda mpaka nafasi ya 5.


MSIMAMO WA VPL.
Kwenye Mabano Idadi ya Mechi Zilizochezwa.
1. Toto Africa (4) 7
2. Simba SC (2) 6
3. JKT Ruvu (3) 5
4. Africa lyon (4) 5
5. Coastal Union (3) 4
6. Moro United (3) 4
7. MtibwaSugar (3) 4
8. Villa Squad (3) 4
9. Azam FC (2) 3
10. JKT Oljoro (2) 3
11. KageraSugar (4) 3
12. PolisiDodoma (3) 2
13. RuvuShooting (2) 1
14. Yanga SC (2) 1