Nov 1, 2011

Tanzania na matatizo katika soka

Kila ukifungu kurasa za wahariri wa habari za michezo utakutana na kichwa cha habari kinachosema tuwekeze katika soka la vijana ili kujikomboa katika soka.

Mara nyingi kauri kama hizi huja pale timu zetu zinapofanya vibaya ila zinapobahatisha kushinda timu hizo hizo husifiwa na suala la kuanzisha timu za vijana wadogo hufa vichwani mwa wahariri na wanaharakati wa soka.

Hata ukitembelea vyama vya soka vya wilaya na mikoa ukiwauliza viongozi wake wanafanya nini ili kuinua viwango vya soka katika eneo lao wao hapo akuna jibu la moja kwa moja utakalopata dhidi ya kujigonga gonga tu .

Mfano leo hii kamuulize katibu wa chama cha soka wilaya yeyote ile nchini je katika wilaya yako kuna timu ngapi zilizosajiliwa na ziko hai hawajui ila mara nyingi huwa wanazilipia timu hada kipindi cha kampeni ili zipate nafasi ya kushiriki katika uchaguzi na kuwachagua wao .

Hebu jiulize kama vyama vyote vya soka kuanzia wilaya na mikoa vingekua makini unadhani tungekupo hapa tulipo sasa katika maendeleo ya soka .

Leo hii hakuna hata chama kimoja cha soka ambacho kimeanzisha japo michuano kwa ajiri ya watoto wadogo under 14  au under 17 lakini cha kushangaza tuna timu ya taifa ya under 17 tff wao wanaitoa wapi hiyo timu kama hiyo timu sio azam fc wanaibadilisha jina tu na hii ndio maana timu zetu za taifa zinakosa uzalendo kutokana na timu moja kujaza wachezaji kisha unaiita taifa staz

 Leo kuna chama kinajiita chama cha kuendeleza soka la vijana kinondoni (KIDIYOSA) lakini nacho hiki kinamapungufu makubwa kila michuano inayoandaliwa na viongozi wa chama hiki sehemu kubwa ya timu zinazoshiliki zinatoka katika kata ya Makumbusho sasa je makumbusho imekuwa wilaya na michuano yenyewe inakosa hata motisha kwa wachezaji wenyewe vijana wanajituma hadi kufika fainali matokeo yake wanapewa kikombe kitupu tena hakina hadhi ya michuano yenyewe nali timu zimetumia gharama kubwa sana katika kushiliki michuano hiyo pia timu ndio huamuliwa kuwalipa waamuzi na wafunga nyavu hivi kuna humuhimu wa kuwa na vyama kama hivi hapa nchini .

Sisi Bonde fc tunapenda kushauli kwa viongozi wa soka na waandishi wa habari wapende kushirikiana na sisi tunaomiliki timu za watoto wadogo kuanzia miaka 7 hadi 21 kwani kuna hadi timu zinashiliki ligi kuu hazina timu za vijana wadogo.

Ukitazama kwa haraka katika wilaya ya kinondoni timu zenye watoto wa kuanzia miaka 8 hadi 21 ni chache sana na zina hali ngumu zimekuwa zikitegemea kuombaomba tu ilizishiliki katika michuano mbalimbali inayozikabili timu hizo ni Bonde Fc, Makumbusho Talent, Shein Rangers, Lion Magomeni, Kimara hizi ndio timu zenye mipango ya muda mrefu basi tunawaomba wadau wa soka kujitokeza kwa kuzisaidia timu hizi na kuacha tabia ya kusubili mchezaji hujui katokea wapi wewe unamsajili matokeo yake timu zinakosa wachezaji wenye nidhamu na wengine kujiona wao ni bora zaidi na hii inatokana na kukosa misingi imara  

Katika kudhibitisha hili tunawakalibisha wadau wotewa soka kuwa wawe wanafika siku za jumapili maeneo ya magomeni barafu kuja kuona timu za under 14 zinavyo oneshana kabumbumbu safi

No comments: