Sep 20, 2011

Kama ulidhani unaujua utani, basi sikia hii

Mwamuzi Howad Webb, anapochaguliwa kuwa mchezaji bora kuwahi kuichezea United.
Katika hali ya kustaajabisha sana, baadhi ya mashabiki wa soka kutoka kona mbalimbali za dunia wamemchagua mwamuzi Howad Webb kuwa ndio mchezaji bora kabisa wa sasa wa kikosi cha Manchester United chini ya kocha Alex Ferguson, ikiwa ni dakika chache sana toka kocha huyo mkongwe kumfananisha mshambuliaji wake Wayne Rooney sawa na gwiji wa soka Pele.
Mashabiki hao wamefanya hivyo kupitia kura ya maoni iliyokuwa ikiendeshwa na mtandao maarufu wa habari za michezo duniani wa TalkSports, ambao katika ukurasa wao wa Facebook, waliendesha kura hiyo kwa kuuliza “Fergie amemfananisha Wayne Rooney na Pele, lakini unadhani ni nani mchezaji bora kabisa wa Manchester United?”
Kwenye kura hiyo, mtandao huo uliainisha majina ya wachezaji kadhaa wakiwemo Bobby Chalton, Ryan Giggs, Eric Cantona, Eric Djemba Djemba, Duncan Edwards, Wayne Rooney, Cristiano Ronaldo, Paul Scholes na wengineo wengi ambapo katika hali ya kustaajabisha wapiga kura walimtaja Howad Webb kama mchezaji bora kwa zaidi ya asilimia 48, akiwaacha mbali kweli magwiji wa ukweli.
Webb alipata asilimia 48, akifuatiwa katika nafasi ya pili na Bobby Chalton (20%), Ryan Giggs akishika nafasi ya tatu.

Kazi kweli kweli…

No comments: