
Uongozi
 wa mabingwa soka Tanzania Bara, Yanga ya jijini Dar es Salaam, 
umeiandikia barua Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuomba 
kiwanja ambacho wanatarajia kujenga uwanja wa kisasa hivi karibuni.
  
Akizungumza
 jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mtendaji wa klabu hiyo, Celestine 
Mwesiga, alisema, wameiandikia barua wizara hiyo, kutaka kupewa kiwanja 
cha hekari 20 katika Manispaa ya Kinondoni au Ilala, ili waweze kutimiza
 ndoto yao ya kutaka kumiliki kiwanja hicho cha kisasa kama ilivyo kwa 
klabu mbalimbali duniani.
  
“Tumeishafanya
 mawasiliano na wenzetu wa Wizara ya Ardhi kuomba kupatiwa kiwanja hicho
 na wameonyesha wapo tayari kutufanikishia lengo letu, hivyo tunasubiri 
wakati wowote watujulishe wapi wametupata,” alisema Mwesiga.
  
Alisema
 uongozi wake umejipanga kuhakikisha unajenga uwanja huo, ili Yanga 
iweze kupunguza gharama mbalimbali zinazolipwa kupitia viwanja 
wanavyochezea sasa, ili waweze kujiimarisha kiuchumi.
  
Akifafanua
 kuhusu uwanja huo, Mwesiga alisema utakuwa na bwawa la kuogelea, uwanja
 wa tenisi, mpira wa mikono, sambamba na hosteli kwa ajili ya wachezaji 
wa klabu hiyo.
  Hivi
 karibuni, watani zao Simba walitangaza mikakati mbalimbali kujenga 
vitega uchumi ikiwamo kujenga jengo la ghorofa 12 yalipo makao makuu ya 
klabu hiyo mtaa wa Msimbazi sambamba na uwanja wa kisasa ‘Simba Sports 
Arena, huko Bunju nje kidogo ya jiji.
chanzo na  http://www.shaffihdauda.com
No comments:
Post a Comment