Dec 14, 2011

Kampuni ya 2F CO.LTD YAJITOSA KUIDHAMINI BONDE KIDS

 Picha juu na china mmoja wa wakurugenzi wa 2F CO.LTD mwenye kanzu akiwa  na viongozi pamoja na wachezaji wa Bonde Fc siku ambapo Bonde fc ilishinda mechi yake ya nusu fainali .
2F CO.LTD imejitolea kuisaidia timu ya Bonde Kids.  Itakuwa ikiisaidia Bonde Kids katika vifaa vya michezo zikiwemo jezi na masuala mbalimbali yanayohusu kuindeleza timu 
Pia kampuni ya 2F CO.LTD kupitia kwa mmoja wa wakurugenzi wake Bwana SALM NGINGO pia imewataka watu wengine wenye uwezo kujitokeza katika kuisaidia timu kwani kusaidia timu kama hizi ndio kusaidia kukuza soka la nchi yetu. Nao uongozi mzima wa Bonde Kids unatoa shukrani kwa kampuni ya 2F CO.LTD kwa uamuzi wao wa kuamua kidhamini timu yao pia wanawaomba watu wenye nia nzuri na soka la vijana kujitokeza kuzisaidia timu kama hizi zenye malengo ya kuinua soka la vijana.

No comments: