Sep 3, 2011

Arsenal yawa klabu ya mfano Ulaya

Michel Platini, raisi wa UEFA ambaye anataka kuona vilabu vinaacha tabia ya kununua mafaanikio kwa kutumia fedha za wafanyibiashar
Wakati mamilioni ya mashabiki wa klabu mbalimbali za soka barani Ulaya wakiendelea kufurahia namna ambavyo timu zao zinamwaga mapesa kwa ajili ya kufanya usajili wa wachezaji wakali na hivyo kuongeza uimara wa vikosi vyao kila msimu wa usajili unavyowadia, Michael Platini, ametangaza  kuwa kiama cha vilabu vyote vinavyonunua mafanikio kwa kutumia jeuri ya fedha za wamiliki wao, kiko palepale na hakikwepeki.
Raisi huyo wa Shirikisho la Vyama vya soka barani Ulaya (UEFA), akiongea kwenye mkutano uliofanyika mjini Zurich jana, alisema kuwa, mpango wa kuvidhibiti vilabu ambavyo vimekuwa vikifanya matumizi makubwa ambayo ni nje ya uwezo wake wa uzalishaji, uko palepale na kwamba utaanza kutumika kwenye msimu wa mwaka 2012/13, kama ambavyo imeshakubaliwa.
Chini ya mpango huo, vilabu havitaruhusiwa kufanya manunuzi ya wachezaji au kulipa mishahara mikubwa kwa wachezaji wao zaidi ya kile klabu inachoingiza kama mapato yake kutokana na mikataba mbalimbali ya kibiashara na vyanzo vyao vya mapato na kwamba vilabu ambavyo vitashindwa kutimiza sharti hilo, vitafungiwa kushiriki michuano yoyote ya Ulaya katika ngazi ya vilabu.
Akizungumza katika mkutano huo, Platini, gwiji wa zamani katika kikosi cha Ufaransa na vilabu mbalimbali alitolea mfano wa klabu ya soka ya Arsenal, ambayo alisema kuwa miaka kumi iliyopita, mzunguko wake wa fedha kwa mwaka ulikuwa chini sana kiasi cha kupitwa na vilabu kama Chelsea, Liverpool na Newcastle, lakini kutokana na mipango mizuri na matumizi sahihi ya fedha, leo hii klabu hiyo imekuwa juu ya vilabu hivyo kwa karibu mara mbili kiuchumi.

No comments: