
Michel
 Platini, raisi wa UEFA ambaye anataka kuona vilabu vinaacha tabia ya 
kununua mafaanikio kwa kutumia fedha za wafanyibiashar
Raisi huyo wa Shirikisho la Vyama vya 
soka barani Ulaya (UEFA), akiongea kwenye mkutano uliofanyika mjini 
Zurich jana, alisema kuwa, mpango wa kuvidhibiti vilabu ambavyo vimekuwa
 vikifanya matumizi makubwa ambayo ni nje ya uwezo wake wa uzalishaji, 
uko palepale na kwamba utaanza kutumika kwenye msimu wa mwaka 2012/13, 
kama ambavyo imeshakubaliwa.
Chini ya mpango huo, vilabu 
havitaruhusiwa kufanya manunuzi ya wachezaji au kulipa mishahara mikubwa
 kwa wachezaji wao zaidi ya kile klabu inachoingiza kama mapato yake 
kutokana na mikataba mbalimbali ya kibiashara na vyanzo vyao vya mapato 
na kwamba vilabu ambavyo vitashindwa kutimiza sharti hilo, vitafungiwa 
kushiriki michuano yoyote ya Ulaya katika ngazi ya vilabu.
Akizungumza katika mkutano huo, Platini,
 gwiji wa zamani katika kikosi cha Ufaransa na vilabu mbalimbali 
alitolea mfano wa klabu ya soka ya Arsenal, ambayo alisema kuwa miaka 
kumi iliyopita, mzunguko wake wa fedha kwa mwaka ulikuwa chini sana 
kiasi cha kupitwa na vilabu kama Chelsea, Liverpool na Newcastle, lakini
 kutokana na mipango mizuri na matumizi sahihi ya fedha, leo hii klabu 
hiyo imekuwa juu ya vilabu hivyo kwa karibu mara mbili kiuchumi.
No comments:
Post a Comment