Sep 3, 2011

Mkali wa Arsenal aanza na hat-trick

Chu-Young Park
Mshambuliaji mpya wa Arsenal Chu-Young Park, amesherehekea kutimia kwa ndoto yake ya kuwachezea washika bunduki hao wa London, kwa kuiongoza nchi yake ya Korea Kusini kuibuka na ushindi wa bao 6-0 dhidi ya Lebanon, katika michuano ya kuwania kufuzu fainali zijazo za kombe la dunia.
Park, ambaye alitua Arsenal hivi karibuni akitokea Monaco ya Ufaransa, aliwaonyesha mashabiki wa Arsenal kuwa huenda akawa tiba ya timu yao kushindwa kupata mabao katika baadhi ya nyakati, baada ya kutikisa nyavu mara tatu kwenye mechi hiyo iliyofanyika leo huko nchini kwao.
Pak, alifunga mabao yake kunako dakika za 8, 45 na 67, huku mabao mengine yakiwekwa nyavuni na Don Won Ji (66 na 85) pamoja na Jung Woo Kim, aliyefunga bao moja kunako dakika ya 82.

No comments: