
Chu-Young Park
Mshambuliaji mpya wa Arsenal Chu-Young 
Park, amesherehekea kutimia kwa ndoto yake ya kuwachezea washika bunduki
 hao wa London, kwa kuiongoza nchi yake ya Korea Kusini kuibuka na 
ushindi wa bao 6-0 dhidi ya Lebanon, katika michuano ya kuwania kufuzu 
fainali zijazo za kombe la dunia.
Park, ambaye alitua Arsenal hivi 
karibuni akitokea Monaco ya Ufaransa, aliwaonyesha mashabiki wa Arsenal 
kuwa huenda akawa tiba ya timu yao kushindwa kupata mabao katika baadhi 
ya nyakati, baada ya kutikisa nyavu mara tatu kwenye mechi hiyo 
iliyofanyika leo huko nchini kwao.
Pak, alifunga mabao yake kunako dakika 
za 8, 45 na 67, huku mabao mengine yakiwekwa nyavuni na Don Won Ji (66 
na 85) pamoja na Jung Woo Kim, aliyefunga bao moja kunako dakika ya 82.
No comments:
Post a Comment